• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • • China kujenga mji wa Shenzhen kuwa eneo la kielelezo cha ujamaa wenye umaalum wa China
     08-19 18:14

    Serikali ya China imetangaza kuunga mkono kuujenga mji wa Shenzhen kuwa eneo la kielelezo cha ujamaa wenye umaalum wa China, ili kusukuma mbele sera ya mageuzi na kufungua mlango, na kutekeleza vizuri zaidi mkakati wa eneo kubwa la ghuba ya Guangdong, Hong Kong na Macao.

    • Uchumi wa China kwa mwezi wa Julai waendelea kukua kwa utulivu
     08-14 17:12

    Takwimu zilizotolewa leo na Idara Kuu ya Takwimu ya China zinaonesha kuwa, mwezi Julai uchumi wa China umeendelea kukua kwa kasi inayofaa. Katika kipindi kijacho, China itaimarisha uhamasishaji wa uvumbuzi kwa uchumi, na kuongeza uhai wa soko, ili kuhimiza uchumi wa China kuendelea vizuri kwa utulivu na mfululizo.

    • Gazeti la The Wall Street Journal la Marekani laonya sera isiyo sahihi ya kibiashara itasababisha kushuka kwa uchumi wa nchi hiyo 08-09 17:25

    Gazeti la The Wall Street Journal la Marekani limetoa tahariri inayoonya juu ya sera isiyo sahihi ya kibiashara iliyotolewa na serikali ya rais Donald Trump wa Marekani, na kusema itasababisha kushuka kwa uchumi wa nchi hiyo.

    • China kupanua masoko ya vijijini 08-05 16:59
    Mkutano wa Ofisi ya Siasa ya Kamati Kuu ya Chama cha Kikomunisti cha China (CPC) kuhusu kazi za uchumi kwa nusu ya pili ya mwaka huu uliofanyika wiki iliyopita umetaka kupanua soko katika sehemu za vijijini. Wasomi nchini China wanasema, wakati China inapopanua mahitaji ya ndani ya nchi, hadhi ya masoko ya vijijini imeanza kuzingatiwa zaidi.
    • Jumuiya ya kimataifa yasifu waraka uliotolewa na China kuhusu mambo ya kihistoria ya Xinjiang
     07-23 17:11

    Ofisi ya habari ya baraza la serikali ya China imetoa waraka wa "masuala ya kihistoria ya mkoa wa Xinjiang", na kukosoa makundi yenye uhasama ya ndani na nje ya China kwa kupotosha historia na ukweli wa mambo ya mkoa huo. Watu wa hali mbalimbali wa jumuiya ya kimataifa wamepongeza waraka huo, wakisema mkoa wa Xinjiang ni sehemu isiyotengeka ya China, na kutokana na sera nzuri ya makabila, mkoa huo umepata ustawi na maendeleo ya mfululizo.
    • Rais wa China azungumza na mrithi wa ufalme wa Abu Dhabi wa Falme za Kiarabu
     07-22 16:45

    Rais Xi Jinping wa China leo hapa Beijing amefanya mazungumzo na mrithi wa ufalme wa Abu Dhabi Sheikh Mohammed bin Zayed Al Nahyan ambaye yupo ziarani nchini China. Rais Xi amesema, uhusiano kati ya nchi hizo mbili ni mfano wa kuigwa wa ushirikiano wa kimkakati kati ya nchi zenye utamaduni na mtindo tofauti na kutoka kwenye kanda tofauti, na China inapenda kushirikiana na Falme za Kiarabu kuhimiza uhusiano huo kupata mafanikio mapya, ili kuwanufaisha wananchi wao.

    • Wawakilishi wa Afrika wasifu umuhimu wa kiujenzi wa China katika sekta ya amani na usalama 07-17 19:56
    Mkutano wa kwanza wa amani na usalama kati ya China na Afrika umefunguliwa tarehe 15 mjini Beijing, na kuhudhuriwa na mawaziri wa ulinzi na wanadhimu wakuu 15 wa majeshi kutoka nchi za Afrika zikiwemo Cameroon na Ghana, wajumbe waandamizi wa nchi 50 za Afrika na idara za ulinzi za Umoja wa Afrika, pamoja na wawakilishi wa jeshi la China. Kwenye ufunguzi wa mkutano huo, wajumbe kutoka Afrika wamesifu mchango wa kiujenzi uliotolewa na China katika sekta ya amani na usalama.
    • Nchi za Afrika zatarajia kuimarisha ushirikiano wa kiusalama na China 07-17 10:37

    Kongamano la Amani na Usalama kati ya China na Afrika linaendelea hapa Beijing, ambapo maofisa waandamizi karibu 100 kutoka nchi 50 za Afrika na idara ya ulinzi ya Umoja wa Afrika pamoja na wajumbe wa jeshi la China wanajadili jinsi ya kuimarisha ushirikiano kati ya pande hizo mbili katika mambo ya amani na usalama.

    • China kuharakisha matumizi ya teknolojia ya juu katika mambo ya bandari
     07-11 19:12

    Leo tarehe 11, Julai ni siku ya safari ya baharini ya China. Naibu waziri mawasiliano ya mawasiliano na uchukuzi wa China Bw. Liu Xiaoming amesema, China imeshika nafasi ya kwanza duniani kwa uwezo wa kupakia na kupakua mizigo na makontena bandarini kwa miaka 16 mfululizo, hata hivyo China bado haina nguvu kubwa katika usafirishaji wa bidhaa baharini. Ameongeza kuwa China itaharakisha matumizi ya teknolojia mpya za juu katika mambo ya bandari.

    • China kuongeza hatua zaidi kutuliza biashara ya nje 07-11 08:39

    Taarifa iliyotolewa jana baada ya mkutano wa watendaji wa Baraza hilo uliloongozwa na waziri mkuu Li Keqiang imesema, ili kutuliza biashara hiyo, ufunguo ni kufungua mlango zaidi na kujikita katika kuboresha nguvu kubwa ya viwanda kupitia mageuzi ya masoko na njia za kiuchumi.

    • China yadumisha utulivu wa bei ya bidhaa
     07-10 19:08

    Takwimu zilizotolewa leo na idara kuu ya takwimu ya China zinaonesha kuwa, mfumuko wa bei nchini China kwa mwezi Juni ulikuwa asilimia 2.7, huku bei ya bidhaa za viwanda ikipungua kwa asilimia 0.3. Wataalam wamesema kiwango cha mfumuko wa bei nchini China kinadhibitika, na bei ya bidhaa itaendelea kwa utulivu.

    • Matumizi ya watu yahimiza maendeleo ya uchumi nchini China
     07-08 16:34

    Takwimu mpya zilizotolewa na Idara kuu ya Takwimu ya China zinaonesha kuwa, katika miaka 70 iliyopita tangu kuanzishwa kwa Jamhuri ya Watu wa China, kipato cha wananchi wa China kimeongezeka kwa mfululizo, huku kiwango chao cha matumizi kikiinuka siku hadi siku. Kwa mujibu wa takwimu hizo, mwaka jana wastani wa matumizi ya kila mchina yalizidi dola 2,880 za kimarekani, ambalo ni ongezeko la mara 19.2 ikilinganishwa na mwaka 1978.

    • Maonesho ya kwanza ya uchumi na biashara ya China na Afrika yafunguliwa
     06-27 18:10

    Maonesho ya kwanza ya uchumi na biashara ya China na Afrika yamefunguliwa leo mjini Changsha, China. Maonesho hayo yenye kauli mbiu ya "ushirikiano kuleta mafanikio ya pamoja, kuhimiza uhusiano wa uchumi na biashara kati ya China na Afrika", yatahusisha shughuli mbalimbali za biashara, uwekezaji, teknolojia za kilimo, nishati, maeneo ya ushirikiano ya viwanda, miundombinu na ushirikiano wa mitaji.

    • China yapinga vitendo vya kujilinda kibiashara huku ikifungua mlango zaidi
     06-27 18:05

    Kutokana na vitendo vya kujilinda kibiashara vinavyoendelea hivi sasa, uchumi wa dunia unakabiliwa na changamoto kubwa. Dunia nzima inatarajia kuwa mkutano wa kilele wa Kundi la Nchi 20 (G20) utakaofanyika mjini Osaka, Japan utaonesha msimamo wazi wa kupinga vitendo hivyo, ili kurejesha uchumi wa dunia kwenye njia sahihi ya maendeleo.

    • Rais Xi Jinping wa China ajibu barua kwa kijana wa Japan 06-26 19:56

    Rais Xi Jinping wa China amejibu barua kutoka mshindi wa mashindano ya Kombe la Panda ya insha ya vijana wa Japan Bw. Nakajima Daiiti, ambaye amemwandikia barua na kumtakia rais Xi kila la heri, na kuonesha matarajio mema ya kazi za urafiki kati ya China na Japan.

    • Ushirikiano wa kunufaishana kati ya China na Afrika ni nguvu ya kuhimiza maendeleo ya dunia
     06-26 18:55

    Mkutano wa waratibu wa kutekeleza matokeo yaliyofikiwa kwenye mkutano wa kilele wa Beijing wa Baraza la Ushirikiano kati ya China na Afrika FOCAC ulifungwa hivi karibuni hapa Beijing, na maonesho ya kwanza ya uchumi na biashara ya China na Afrika yatafunguliwa kesho mjini Changsha, China.

    • China yapiga hatua katika juhudi za kuondoa umaskini kwenye sehemu zenye umaskini uliokithiri
     06-26 17:07

    Ofisa mwandamizi wa ofisi ya kuwasaidia watu maskini iliyo chini ya baraza la serikali la China Bw. Ou Qingping amesema, China imeongeza nguvu katika kuondoa umaskini kwenye sehemu zenye umaskini uliokithiri, na hatua ijayo itakuwa ni kuhamasisha matumizi kuwa njia muhimu ya kuondoa umaskini.

    • Mkutano wa waratibu wa kutekeleza matokeo ya mkutano wa kilele wa Beijing wa FOCAC wafanyika
     06-25 16:30

    Mkutano wa waratibu wa kutekeleza matokeo yaliyofikiwa kwenye mkutano wa kilele wa Baraza la Ushirikiano kati ya China na Afrika FOCAC umefanyika leo hapa Beijing. Rais Xi Jinping wa China ametuma salamu za kupongeza mkutano huo, akitaka China na Afrika zichukue mkutano huo kama fursa mpya ya kujenga kwa pamoja "Ukanda Mmoja, Njia Moja", kuboresha maisha ya watu bilioni 2.6 wa China na Afrika, na kujitahidi kujenga jumuiya ya China na Afrika iliyo karibu zaidi na yenye mustakabali wa pamoja.

    • Rais wa China kuhudhuria mkutano wa Kundi la Nchi 20
     06-24 16:55

    Rais Xi Jinping wa China anatarajiwa kuhudhuria mkutano wa 14 wa kilele wa kundi la nchi 20 (G20) kuanzia tarehe 27 hadi 29 utakaofanyika mjini Osaka, Japan. Hii itakuwa mara ya saba mfululizo ya rais Xi kuhudhuria mkutano huo.

    • Marekani yaweka vigezo tofauti katika ulinzi wa hakimliki
     06-19 10:10

    Mbunge wa baraza la seneti la bunge la Marekani Marco Rubio ametoa mswada wa kusahihisha sheria ya ulinzi, kwa kulenga kupiga marufuku Kampuni ya Huawei ya China kudai malipo ya hataza kwa makampuni ya Marekani.

    prev 1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 next
    SearchYYMMDD  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako